Wayan Mirna Salihin mwenye umri wa miaka 27, alifariki dunia mjini Jakarta mapema mwzi huu baada ya kunywa kahawa na rafiki zake wanaojulikana kwa majina ya Jessica Kumala and Hani.
Inaaminika kuwa, kinywaji chake kiliwekewa sumu aina ya cyanide.
Kufuatia wiki kadhaa za upelelezi, polisi wa Jakarta, leo hii wamemkamata Bi Jessica Kumala.
Mabinti hao watatu walisoma pamoja masuala ya ubunifu, katika chuo cha Billy Blue mjni Sydney na pia chuo kikuu cha Teknolojia Swinburne huko Melbourne.
Imeelekwa kuwa Polisi wa shirikisho Australia wameliambia jeshi la Polisi Jakarta watatoa msaada wa ushirikiano kusaidia kesi hiyo.

