Afrika yaomboleza kifo cha mfalme wa Afro-Jazz

Msanii maarufu nchini Zimbabwe na barani Afrika na duniani kote Oliver 'Tuku' Mtukudzi, ame aga dunia akiwa na umri wa miaka 66, baada ya kutawala mziki wa Afro-Jazz kwa zaidi ya miongo minne.

Mfalme wa Afro-Jazz Oliver Mtukudzi, kwenye tamasha

Mfalme wa Afro-Jazz Oliver Mtukudzi, kwenye tamasha Source: AAP

Tuku alikuwa mmoja wa walio pinga uongozi wa wazungu nchini Zimbabwe, na mara nyingi nyimbo zake zilikuwa na ujumbe kwa jamii. Ujumbe huo ulijumuisha ushauri kuhusu virusi vya ukimwi, na nyimbo zake pia zilikuwa na ujumbe ficho ulio kosoa serikali, hatua iliyo sababisha baadhi ya nyimbo zake kupigwa marufuku nchini humo.

Tuku alikuwa muimbaji na mpigaji gita aliye changanya aina tofauti ya miziki, naku unda aina ya muziki iliyo julikana kama Afro-jazz na mashabiki wengi wa muziki wake wali ita aina hiyo ya muziki, "Tuku Music".

Katika safari yake ndefu kimziki, Tuku alitoa albamu 67 naku fanya ziara duniani kote, Australia ikijumuishwa ambako alitumbuiza mashabiki wake kwa mara ya mwisho mwaka wa 2015.

Mfalme wa Afro-Jazz Oliver Mtukudzi, kwenye tamasha
Mfalme wa Afro-Jazz Oliver Mtukudzi, kwenye tamasha Source: EPA

Oliver Mtukudzi, atakumbukwa kwa wimbo wake maarufu kwa jina la Neria, ambao ulitetea usawa wa jinsia.

 


Share

1 min read

Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service