Breaking

Afrika ya mkumbuka Baba

Tangazo la kifo cha Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya na Kinara wa chama cha upinzani cha ODM, Raila Odinga limetikisa bara la Afrika.

Raila Odinga

Kenyan opposition leader Raila Odinga lifts his hat to thousands of supporters gathered at a rally in the Shauri Moyo area of Nairobi, Kenya, Wednesday, Oct. 18, 2017. Source: AP / Ben Curtis/AP/AAP Image

Rais wa Kenya Dkt William S Ruto, akiwa pamoja na Dkt Oburu Odinga (kakake Raila) alitoa hotuba fupi aki tangaza rasmi kifo cha Kinara wa chama cha upinzani cha ODM Raila Odinga ambaye anajulikana pia kama "Baba."

Kwa mujibu wa maelezo ya daktari aliye mhudumia Baba, kilicho sababisha kifo chake ilikuwa ni mshutuko wa moyo aliopata alipokuwa akitembea ndani ya pango aliko kuwa akipata huduma ya afya nchini India.

Mwili wa Baba unarejeshwa nchini Kenya ukisindikizwa na baadhi ya viongozi wakiwemo Kiongozi wa Mawaziri wa Kenya Musalia Mudavadi, na Katibu Mkuu wa ODM, Edwin Sifuna miongoni mwa viongozi wengine.

Mwendazake alikuwa ameomba azikwe ndani ya masaa 72 baada ya kuaga dunia, ila kwakuwa mauti yalimkuta nje ya nchi pamoja na taratibu za maandalizi ya mazishi, serikali imetangaza kuwa Baba pewa pumziko la mwisho Jumapili kando ya kaburi la mamake.

Tuta waletea taarifa zaidi punde tutakapo zipokea.

Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service