Anthony Albanese, Waziri Mkuu wa 31 wa Australia

Baada ya takriban wiki sita za kampeni ngumu zilizo shuhudiwa kote nchini, hatimae uchaguzi mkuu umefanyika na upinzani kuibandua serikali ya mseto madarakani.

Kiongozi wa Upinzani Anthony Albanese awashukuru wanachama wenza baada ya hotuba yake.

Kiongozi wa Upinzani Anthony Albanese awashukuru wanachama wenza baada ya hotuba yake. Source: AAP

Waziri Mkuu Scott Morrison, alihotubia taifa usiku wa Jumamosi 21 Mei 2022 nakutoa shukrani zake za dhati kwa taifa na washiriki wake kwa muda alio ongoza nchi.

Katika hotuba yake Bw Morrison alisema pia kuwa alikuwa amezungumza na kiongozi wa upinzani Bw Albanese nakumpongeza kwa kushinda uchaguzi mkuu. Licha yakuwa hesabu za kura bado zina endelea, hakuna uwezekano wa chama cha mseto kuweza kuunda serikali.

Bw Anthony Albanese alishukuru taifa kwa kumpa heshima yakuongoza taifa, pamoja nakumshukuru mtangulizi wake Bw Morrison kwa huduma aliyotoa kwa taifa. SBS Swahili itachapisha matokeo kamili ya uchaguzi mkuu, punde tutakapo yapata.

 

 


Share

Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Anthony Albanese, Waziri Mkuu wa 31 wa Australia | SBS Swahili