Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Takribani watu 47 wafariki dunia katika ajali ya basi nchini Zimbabwe

Taarifa zinaelezea kuwa watu 47 wamefariki nchini Zimbabwe baada ya mabasi mawili kugongana.

Library photo bus crash
Libeary photo bus crash Source: RSS

Takribani watu 47 wamefariki baada ya mabasi mawili kugongana uso kwa uso Kaskazini-Mashariki nchini Zimbabwe, kituo cha runinga ya taifa kilieleza.

Ajali hiyo ilitokea siku ya Jumatano karibu na mji wa Rusape, kwa mujibu wa shirika la utangazaji la Zimbabwe.

Miongoni mwa waliofariki ni watu wazima 45 na watoto wawili, alikaririwa akisema msemaji wa polisi Paul Nyathi.

 Mabasi hayo yalikuwa yakisafiri kati ya mji mkuu Harare, na mji wa Mutare.

Kama ilivyo kwa mataifa mengi ya Afrika, ajali za barabarani zimekuwa za kawaida nchini Zimbabwe kutokana na miundo mbinu mibovu ya barabara na uhaba wa magari ya uhakika.

Tutawaletea habari zaidi.


1 min read

Published

By Frank Mtao

Presented by Frank Mtao

Source: AAP



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now