Australia kuwakatalia visa wahalifu wa unyanyasaji majumbani

Australia itakataa kutoa visa kwa watu wenye hatia ya ukatili.

Immigration Minister David Coleman.

Immigration Minister David Coleman. Source: SBS

Wageni wa Australia wanaweza kukataliwa kuingia au kufukuzwa nje ikiwa wamehukumiwa kwa unyanyasaji wa majumbani, chini ya maagizo ya serikali mpya ya shirikisho.

Uamuzi wa Waziri wa Uhamiaji David Coleman ulianza kutumika Alhamisi, kuzuia mtu yeyote ambaye amefanya vurugu dhidi ya wanawake au watoto hapa nchini.

"Ikiwa umehukumiwa na kosa la uhalifu dhidi ya wanawake au watoto, hamkubaliki," Mr Coleman alisema.

"Popote ambapo kosa limetokea, hukumu yoyote, Australia haitakuwa na uvumilivu kwa wahalifu wa majumbani."

Alisema mwelekeo huo utatumika sio tu kwa watunga maamuzi ndani ya Idara ya Mambo ya Ndani, lakini pia kwa Mahakama ya Rufaa ya Utawala. 

"Kumekuwa na idadi kadhaa ambapo waamuzi katika serikali wamekataa visa kwa mtu aliyekuwa na hatia ya unyanyasaji wa nyumbani.


Share

Published

By Frank Mtao
Presented by Frank Mtao

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service