Australia yatinga fainali ya kombe la dunia

Timu ya taifa ya Australia imekuwa kambini nchini Qatar, kwa zaidi ya wiki mbili ikijiandaa kucheza dhidi ya Peru kwa haki yakucheza katika kombe la dunia baadae mwaka huu.

Aussies qualificam-se para o Mundial de futebol no Catar

Aussies qualificam-se para o Mundial de futebol no Catar Source: @Socceroos twiteer

Katika muda huo, Australia ilicheza dhidi ya timu ya Falme zakiarabu nakuibuka mshindi kwa magoli mbili kwa moja nakusogea hatua mbele kushiriki katika mechi dhidi ya Peru itakayo amua timu ya mwisho itakayo shiriki katika kombe la dunia baadae mwaka huu.

Alfajiri ya leo 14 Juni 2022, Australia ili ingia dimbani dhidi ya Peru katika mechi iliyo kuwa na nafasi chache kwa timu zote kufunga goli. Dakika za kwanza tisini ziliisha bila mshindi, na katika dakika za nyongeza hazikutosha kwa pande yoyote kupata ushindi hatua iliyo salia ilikuwa penati kuamua mshindi.

Australia ili ibuka mshindi wa magoli tano kwa nne dhidi ya Peru, nakujikatia tiketi yakucheza katika kombe la dunia nchini Qatar.


Share

Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service