Australia ili ingia uwanjani dhidi ya Denmark ikijua lazima ishinde mechi yake la sivyo ushiriki wao katika Kombe la Dunia utakuwa mashakani.
Kama ilivyo tarajiwa nakutabiriwa, Denmark ilimiliki mpira kwa muda mrefu, ila hiyo yote haikutosha kutikisa walinzi wa Australia katika mechi hiyo. Na katika dakika ya 60, nyota wa Melbourne City FC, Mathew Leckie aliwakwepa walinzi wa Denmark nakufyatua kombora kwa mguu wake wakushoto hadi ndani ya wavu wa Denmark.

Mathew Leckie (2L) of Australia celebrates with teammates after scoring the 1-0 during the FIFA World Cup 2022 group D soccer match between Australia and Denmark at Al Janoub Stadium in Al Wakrah, Qatar, 30 November 2022. EPA/Rolex dela Pena Source: EPA / Rolex dela Pena/EPA
Australia sasa inajiandaa kukabiliana na mtihani mgumu kutoka Lionel Messi na Argentina alfajiri ya Jumapili kwa masaa yamashariki Australia.