Cahill aokoa Australia tena

Socceroos wa Australia walicheza mechi yakufuzu kwa kombe la dunia la 2018 dhidi ya Syria wakijua kwamba, sare yakuto fungana au ushindi ndio utatosha kuwafikisha katika hauta ya mwisho ya michuano yakufuzu.

Tim Cahill asherehekea goli lake la ushindi dhidi ya Syria

Tim Cahill asherehekea goli lake la ushindi dhidi ya Syria Source: AAP

Licha ya Australia kuanza mechi kwa kasi dhidi yawa Syria, wageni ndio walio funga goli ya kwanza katika dimba hilo. Kosa la Mark Milligan katikati ya uwanja lili adhibiwa kwa mkwaju wa Omar Al Soma wa Syria aliye funga goli la kwanza la mechi hiyo.

Socceroos wali endelea kushambulia lango la Syrian na hatimae suluhu iliwasili kupitia krosi ya Matthew Leckie, ambayo ilipokewa kwa furaha na Tim Cahill, ambaye hakusita kuuvunja moyo wa mlinda lango la Syria kwaku funga goli kwa kichwa.

Mechi hiyo ilikamilika kwa sare ya 1-1 na punde baada ya mechi kuanza katika dakika 30 za nyongeza, mzigo wa Socceroos uliregezwa baada ya mchezaji wa Syria, Mahmoud Al Maowas kuonesha kadi nyekundu nakuondolewa uwanjani.

Mshindi wa mechi hiyo aliamuliwa katika kipindi cha pili cha dakika 30 za nyongeza, kupitia goli la pili la Tim Cahill katika dakika ya 106. Ila kabla ya mwamuzi kupuliza kipenga cha mwisho, matumaini ya Australia na Syria yalisalia katika miguu ya Omar Al Soma katika dakika ya 120 aliye pewa fursa yaku chambua kitendawili hicho.

Hesabu ilikuwa rahisi, akifunga goli Syria itaendelea katika hatua ya mwisho yakufuzu na Australia ina aga michuano hiyo, ila asipo funga goli hilo basi Syria ndiyo ita aga michuano hiyo. Mamilioni yama shabiki kutoka pande zote walipokuwa wakimwomba Maulana aingilie kati, mkwaju wa Omar Al Soma aligonga mwamba nakuzua shangwe na vigelegele toka kwa mashabiki wa Socceroos, wakati mashabiki wa Syria walisalia na maswali chungu nzima.

Australia sasa ita subiri kujua ni nani kati ya Panama au Honduras atakaye menyana naye, katika hatua ya mwisho yakufuzu kwa kombe la dunia nchini Urusi.

 


Share

1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service