Mamlaka yazima vyombo vya habari Kenya

Mamlaka ya mawasiliano ya Kenya imefunga runinga za Citizen TV, NTV na KTN. Vyombo hivyo vya habari kwa sasa vina peperusha matangazo tu kupitia mtandao.

runinga ya pata matatizo yakuonesha picha vizuri

runinga ya pata matatizo yakuonesha picha vizuri Source: ACMA

Hatu hiyo imejiri wakati wafuasi wa muungano wa upinzani wa National Super Alliance (NASA), wanaendelea kuwasili katika bustani ya Uhuru ambako vinara Raila Odinga na naibu wake Kalonzo Musyoka wata apishwa.

Supporters hand NASA principle Raila Odinga bible for swearing in ceremony
Wafuasi wa NASA wampa Biblia kinara wao Raila Odinga kwa ajili yaku apishwa Source: NASA Kenya
Taarifa zilikuwa zimesambaa katika vyombo vya habari na mtandaoni kuhusu onyo toka kwa serikali kwa wawakilishi wa vyombo vya habari nchini humo ambao walikuwa wame alikwa kwa mkutano maalum ndani ya ikulu mjini Nairobi. Imeripotiwa kuwa serikali ilionya vyombo vya habari dhidi yakupeperusha picha na matangazo ya moja kwa moja ya hafla hiyo ya uapisho. Kufungwa kwa matangazo ya vyombo hivyo vya habari kuna zungumziwa mjini Nairobi, kama adhabu ya serikali kwa vyombo hivyo vya habari ambavyo havija tii amri ya serikali. Image

Chama cha wahariri wa habari nchini Kenya kimekosoa amri ya Ikulu yakuto peperusha picha za hafla ya uapisho wa upinzani.

SBS Swahili ita endelea kukupasha taarifa ya matukio ya uapisho wa vinara wa upinzani kutoka bustani ya Uhuru mjini Nairobi, punde tutakapo pata taarifa hizo.


Share

1 min read

Published

Updated

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service