Taarifa Mpya ya UVIKO-19: Kesi za Omicron za ongezeka Australia

Hii ni taarifa yako mpya kuhusu Coronavirus Australia kwa 7 Disemba 2021

Yvette D'Ath Waziri wa Afya wa Queensland

Waziri wa Afya wa Queensland Yvette D'Ath, asema wanataka kila mtu awe na krismasi salama pamoja na wapendwa wao. Source: AAP Image/Darren England

  • Watu 180 wanao husishwa na shule moja Canberra, wamelazimishwa kujitenga kwa sababu ya hofu kuhusu kuwa hatarini kuambukizwa virusi vya Omicron.
  • NSW imerekodi kesi sita mpya za Omicron, hali ambayo imepelekea idadi ya maambukizi ya aina hiyo mpya ya kirusi kufika 31.
  • Kuanzia 17 December, watu ambao hawaja chanjwa watapigwa marufuku kutoka sehemu zisizo mhimu zakibiashara jimboni Queensland. 
  • Waziri wa afya wa Queensland ametoa taarifa kuwa, kesi chanya iliyo tambuliwa mjini Gold Coast inaungwa na kituo cha huduma ya wazee ila, kwa sasa hakuna mtu mwingine ndani ya makazi hayo ambaye amepatwa na maambukizi hayo.
  • Uchunguzi kutoka shirika la Australian Red Cross umepata kuwa mtu mmoja kati ya watu watatu, hawatazamii msimu wa sherehe waki ulinganisha na miaka ya nyuma na 61%, wana wasiwasi kuhusu jamaa wao ambao wako katika hali mbaya na rafiki zao ambao wana upweke, iwapo vizuizi vya usafiri vita salia.
TAKWIMU ZA UVIKO-19: 

Victoria imerekodi kesi mpya 1,185 ndani ya jamii pamoja na vifo saba.
NSW imerekodi kesi mpya 260 ndani ya jamii pamoja na vifo viwili. 
ACT imerekodi kesi mpya tatu, nayo Queensland imerekodi kesi moja.

Kwa hatua zilizopo kwa sasa katika jibu la janga la UVIKO-19 katika lugha yako, bonyeza hapa



Karantini na vizuizi jimbo kwa jimbo:

Safari

Taarifa kwa wasafiri wakimataifa na UVIKO-19 na taarifa za safari katika lugha yako

Msaada wakifedha

Kuna mageuzi kwa malipo ya janga ya UVIKO-19, punde majimbo yatakapo fikia kiwango cha 70% na 80% ya watu ambao wamepata chanjo kamili: Kupata msaada wakati wa UVIKO-19 kutoka kwa Services Australia katika lugha yako



 


 





Tembelea rasilimali zilizo tafsiriwa nakuchapishwa na shirika la NSW Multicultural Health Communication Service:


Zahanati za vipimo katika kila jimbo na wilaya:

NSW 
ACT 

Share

Published

By SBS/ALC Content
Presented by Gode Migerano
Source: SBS

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service