Uchaguzi wa urais wa DR Congo wa ahirishwa hadi 30 Disemba 2018

Uchaguzi wa urais uliokuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu katika Jamuhuri yakidemokrasia ya Congo, ambao ulistahili fanywa jumapili 23 Disemba, kwa sasa ume futwa naku ahirishwa hadi tarehe 30 Disemba 2018.

Rais wa tume huru ya uchaguzi ya DR Congo, atoa taarifa kuhusu uchaguzi mkuu

Corneille Nangaa Yobeluo, rais wa tume huru ya uchaguzi ya DR Congo, atoa taarifa kuhusu uchaguzi mkuu. Source: Corneille Nangaa Yubeluo

Kiongozi wa tume huru ya uchaguzi ya DRC (CENI) Corneille Nangaa, alieleza taaifa na waandishi wa habari kuwa, tume hiyo haikuwa tayari kufanya uchaguzi huo baada ya mashine za uchaguzi kuteketea katika moto ulio choma jengo ambalo vilikuwa viki hifadhiwa ndani.

Bw Nangaa aliongezea kuwa "Uchaguzi wa urais, bunge pamoja na uchaguzi wa mikoa utafanywa tarehe 30 Disemba, 2018,"

Kwa mujibu wa taarifa kutoka CENI, wiki jana asilimia 80 ya mashine za kura ziliteketezwa kwa moto ndani ya jengo moja mjini Kinshasa. Tukio hilo lime athiri uwezo wa CENi kuhakikisha kura zitapigwa nchini kote siku ya uchaguzi, ndipo tume hiyo ika amua kuahirisha uchaguzi mkuu hadi tarehe 30 Disemba.

SBS Swahili ina andaa mjadala maalam kuhusu uchaguzi wa urais wa DR Congo, mjadala huo uta anza saa tisa mchana kwa masaa ya mashariki ya Australia, Jumapili 23 Disemba 2018.


Share

1 min read

Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service