Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Eve "Kama mama anapitia matatizo, yatamfikia mtoto pia"

Swala la Unyanyasaji wa Nyumbani limekuwa doa kwa jamii nyingi nchini Australia, na taarifa za unyanyasaji wa nyumbani zimendelea kutawala vyombo vya habari hivi karibuni.

If you are experiencing violence, report it to the police
If you are experiencing violence, report it to the police Source: AAP

Wanaharakati na mashirika ambayo hutoa huduma kwa wahanga na waathiriwa wa visa vya unyanyasaji wa nyumbani, wamesisitiza kuwa janga la COVID-19 limeongeza hatari ya swala hili haswa kama watu hawatambui dalili na ishara za visa vya unyanyasaji wa nyumbani.

Rosemary Kariuki ni mwanaharakati wa jamii, alikuwa mzungumzaji kwenye uzinduzi waripoti maalum kuhusu unyanyasaji wa nyumbani, ambayo iliandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chuo cha Western Sydney na shirika la Great Lakes Agency for Peace International (GLAPD). Alipozungumzia swala hili alifafanua nakuweka wazi dalili na ishara za unyanyasaji wa nyumbani akitomfano kuwa ni: "saa zote ukiongea nasima anataka jua unaongea na nani, ukitaka enda omba kanisani au katika msikiti unao penda, anataka tu uende kwa yake, hataki utembelee wala utembelewe na marafiki, ukipika chakula ambacho hapendi hiyo ni kelele". Image

Wanawake wengi na baadhi ya wanaume, wamejipata katika hali kama hizo zilizo elezewa na Bi Rosemary. Wengi wao wakisalia namakovu yakisaikolojia ambayo huwa yana chukua muda mrefu sana kupona.

Bi Eve ni mfanyakazi wa jamii katika shirka la Great Lakes Agency for Peace International (GLAPD), alipozungumzia hoja hii aliwahamasisha wanawake kwa wanaume wanao kabiliwa kwa matatizo ya unyanyasaji wa nyumbani kuwa; "usiteseke mwenyewe, haijalishi unakotoka njoo kwetu tutakupa usaidizi, ukitueleza unachopitia tutakusaidia aau kukutuma sehemu unaweza saidiwa zaidi. Kama mama anapitia matatizo hayo, yatawafikia watoto pia na hatutaki wapitie haya maneno".

Iwapo wewe au mtu unaje jua anapitia changamoto hizo za unyanyasaji wa nyumbani, unaweza pata msaada kwaku wasiliana na masharika yafuatayo: Jeshi la polisi sehemu unako ishi, Relationships Australia (1300 364 277), 1800Respect (1800 737 732), Lifeline (13 11 14), Whiteribbon (08 6370 0600). Taarifa kuhusu mashirika mengi zaidi ambayo yanaweza kusaidia, unaweza ipata mtandaoni. Unaweza wasiliana na viongozi wako wakidini pia kwa msaada na jeshi la polisi unako ishi.


1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now