Hofu kubwa yatanda baada ya taarifa kuibuka kwa Gonjwa la Ebola nchini Congo

Kulipuka Kwa Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumeenea zaidi maeneo ya mji wa Mbandaka, ambapo hofu ya virusi hivyo hatari vimekuwa tishio kubwa kwa ukanda huo.

Ebola

WHO on 10 May 2018 said that 32 Ebola virus disease cases, including 18 deaths, were reported from Bikoro health zone, Equateur. Source: EPA/AHMED JALLANZO

Wataalmu wa afya wanasema, mlipuko huo hatari wa Ebola ulianzia vijijini nchini humo, umetawanyika hadi mjini hivyo kuzua hofu kubwa katika ukanda huo.

Mlipuko mpya umetangazwa rasmi tarehe 8 Mei ikiwa vimefikia vifo 23 hadi sasa, lakini mwanzo mlipuko huo ulitangazwa kutokea vijijini sehemu ya jimbo la Equateur, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.
People suspecting of  Ebola Virus wait at a  treatment centre in Bikoro Democratic Republic of Congo.
People suspecting of Ebola Virus wait at a treatment centre in Bikoro Democratic Republic of Congo. Source: AAP
Lakini wizara ya afya nchini humo na Shirika la Afya Duniani (WHO) siku ya Alhamis walisema, wamethibitisha mlipuko wa gonjwa hilo kuwepo Mbandaka, ambao ni mji mkuu wa Equateur kama kilomita 150 (90 miles) kutoka eneo la Bikoro ambapo mlipuko ulipoanzia.

Madaktari wa kujitolea wajulikanao kama ’Doctors Without Borders (MSF)’, waliwanukuu maafisa wa eneo hilo wakisema, takribani watu 514 wanaaminika kukutana na wagonjwa wa Ebola na kwa sasa wako chini ya uangalizi.

Peter Salama, msimamizi wa masuala ya dharura kutoka WHO, amesema kuenea kwa ugonjwa huo mjini, kunayanya iwe ngumu kupambana nao, kitu kitakachotegemea kutambua na kutenga wanaoshukiwa kupata maradhi.
imagejpeg
Idadi ya watu katika mji wa Mbandaka kwa mujibu ya makadirio yaliyopita ni watu takribani 700,000 hadi milioni 1.2.

Katika msimu uliopita, milipuko mingi ya Ebola nchini DRC, ilikuwa ikitokea vijijini na ilikuwa rahisi kupambana nao lakini kwa sasa tuna zaidi ya milioni moja wako kwenye hatari ya gonjwa," alisema Salama mjini Geneva.

WHO wametangaza kutuma wataalamu 30 kwenye mji wa Mbandaka, wkaati MSF nao walisema, watatuma tani kadhaa za madawa kama sehemu ya msaada kuoambana na janga hilo.


Share

2 min read

Published

Updated



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service