Hatimae michezo ya Olimpiki ya 2020 yaanza mjini Tokyo, Japan

Michezo ya Olimpiki ime anza rasmi mjini Tokyo, Japan baada ya mlipuko wa janga la COVID-19 mwaka jana kuwalazimisha wenyeji na shirika la michezo ya olimpiki kuahirisha michezo hiyo.

Wachezaji wawasili ndani ya ukumbi wa uzinduzi wa michezo ya Olimpiki ya 2020 mjini Tokyo, Japan.

Wachezaji wawasili ndani ya ukumbi wa uzinduzi wa michezo ya Olimpiki ya 2020 mjini Tokyo, Japan. Source: AAP Image/Joe Giddens

Wanaspoti kutoka nchi washiriki duniani kote, walijumuika ndani ya uwanja wa Olimpiki mjini Tokyo, katika hafla ya uzinduzi wa michezo hiyo.

Michezo ya Olimpiki Tokyo 2020
Wapeperushaji wa bendera ya Australia Cate Campbell na Patty Mills waongoza wachezaji wa Australia katika sherehe ya uzinduzi ya michezo ya Olimpiki, Tokyo 2020 Source: Visual China Group via Getty
Tofauti na uzinduzi wa michezo ya Olimpiki ya kabla ambako maelfu yamashabiki walijaa ndani ya uwanja wa michezo na hata nje ya uwanja kushuhudia uzinduzi huo, uzinduzi wa Tokyo 2020 ulifanyika bila mashabiki kwa sababu ya hofu ya usambaaji wa virusi vya COVID-19.

Watu wengi walikuwa na hofu kuwa michezo hiyo ita ahirishwa au kufutwa tena, baada ya ongezeko ya visa vya maambukizi ya COVID-19 nchini Japan, pamoja na katika nchi ambako baadhi ya wachezaji husika wanatoka.

Thomas Deng nahodha wa timu ya mpira wa miguu ya Olimpiki ya Australia
Thomas Deng nahodha wa timu ya mpira wa miguu ya Olimpiki ya Australia, Source: Getty Images

Wanachama wa jamii ya Afrika Mashariki waliwakilishwa kwa fahari na kijana wao, Thomas Deng aliye zaliwa mjini Nairobi, Kenya ambako familia yake walikuwa wakimbizi kutoka Sudan Kusini.

Thomas na familia yake waliwasili nchini Australia, akiwa na miaka sita na sasa ndiye nahodha wa timu ya taifa ya mpira wa miguu ya olimpiki. Thomas aliongoza timu yake kupata ushindi, dhidi ya wababe wa soka duniani Argentina katika mechi ya kwanza ya kundi lao mjini Tokyo, Japan.

Idhaa ya Kiswahili itaendelea kukupa taarifa kuhusu matokeo ya michezo ya Olimpiki ya 2020 kutoka mjini Tokyo, Japan.


Share

Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Hatimae michezo ya Olimpiki ya 2020 yaanza mjini Tokyo, Japan | SBS Swahili