Hatimae wajasiriamali wavuta pumzi ya afueni

Mwaka huu umekuwa mgumu sana, na wenye changamoto nyingi kwa baadhi ya wajasiriamali kote nchini.

Mmiliki wa biashara aweka bango lakueleza wateja biashara imefunguliwa.

Mmiliki wa biashara aweka bango lakueleza wateja biashara imefunguliwa. Source: Getty Images

Wengi wao wamekabiliana na maswali na maamuzi magumu, kuhusu hatma ya biashara zao wakati ambapo mamlaka katika kila jimbo na mkoa nchini wana endelea kuregeza nakukaza vizuizi vyakudhibiti usambaaji wa maambukizi ya virusi vya UVIKO-19.

Katika jimbo la Kusini Australia, mjasiriamali Martin ali eleza idhaa ya Kiswahili ya SBS Kwamba "alikuwa amefika mwisho wa uvumilivu kiasi kwamba aliamua kuacha biashara yake nakutafuta kazi katika sekta nyingine kwa ajili yakumudu gharama za familia yake". Ila baada ya mamlaka husika kuregeza vizuizi kwa mikusanyiko namatukio katika jamii, Bw Martin amefufua biashara yake tena yaku tengeza filamu nakupiga picha za harusi na katika matukio mengine.
Young Martin akiwa kazini
Young Martin akiwa kazini Source: Young Martin

Nako Jimboni Victoria, Bw Tony ambaye biashara yake yakuwasaidia watu kufanya mazoezi baada yakupata jeraha au kwa wanao taka boresha afya yao imijipata katika njia panda. Serikali ya jimbo hilo imetoa ruhusa kwa biashara ndogo kuanza kuwahudumia wateja tena, ila ni wateja walio pata chanjo tu ndiwo wanao ruhusiwa kuhudumiwa. Licha yakupewa idhini yakufungua milango ya biashara yake tena, Bw Tony amesalia na maamuzi magumu kwa jinsi yakuwaeleza baadhi yawateja wake kuwa "hawawezi pokea huduma kwa sababu ya hali yao ya chanjo".

Image

Na jimboni New South Wales, hali imekuwa chanya kwa Mdm Youvip. Biashara yake yakutengeza video nakupiga picha za matukio ilikuwa inaelekea pabaya kabla kiongozi wa jimbo hilo, atangaze ruhusa ya biashara kama zake kuanza kazi tena. Mdm Youvip, alifunguka kuhusu masaibu aliyo kabiliana nayo kama mjasiriamali wakati wa vizuizi vya UVIKO-19.

Mdm Youvip akiwa kazini
Mdm Youvip akiwa kazini Source: Mdm Youvip

Bonyeza hapo juu kwa makala kamili.

 


Share

Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Hatimae wajasiriamali wavuta pumzi ya afueni | SBS Swahili