Helikopta yaua 18 nchini Ethiopia

Wanajeshi kumi na tano na watu wengine watatu, wamefariki dunia baada ya helikopta ya kijeshi kuanguka nchini Ethiopia wakati ikiwa njiani kuelekea mji wa Bishoftu, kusini mwa Addis Ababa.

Crash bodybag (Library photo)

Source: Getty

Helikopta ya kijeshi ilipata ajali eneo la mkoa wa Oromiya nchini Ethiopia, na kuua watu wote 18, ikiwa ni pamoja na askari 15, taarifa ya shirika la habari la serikali la Fana lilitaarifu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Fana, watu hao wengine watatu waliofariki katika ajali hiyo, walikuwa ni raia.

Waziri wa baraza la mawaziri wa mkoa wa Oromiya, Addisu Arega alithibitisha ripoti ya Fana na akaandika hivi: "Abiria wote walifariki dunia, sababu ya ajali hiyo bado inafanyiwa uchunguzi. Tunawapa pole wafiwa wote."

Helikopta ilikuwa ikisafiri kutoka mji wa Mashariki wa Ethiopia wa Dire Dawa na kuelekea Bishoftu karibu na kilomita 60 kusini mwa mji mkuu Addis Ababa, alinukuliwa akisema waziri huyo Bwana Addisu.


Share

1 min read

Published

Updated

By Frank Mtao

Presented by Frank Mtao




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service