Mahakama kuu yawa furusha wanasiasa wakitaifa ofisini

Mahakama kuu ime amua kwamba Barnaby Joyce na wanasiasa wenza wanne ambao wame husishwa katika utata wa uraia pacha, hawastahili kuwa bungeni. Hata hivyo, wawili wengine wame ponea katika uamuzi huo wa mahakama kuu.

Utata wa uraia pacha

Utata wa uraia pacha Source: AAP

Wanasiasa wakitaifa watano naibu waziri mkuu wa zamani Barnaby Joyce akijumuishwa, wamefurushwa ofisini baada ya mahakama kuu kutoa uamuzi wake kwa kesi ya wanasiasa walio kuwa wame kumbwa kwa utata wa uraia pacha.

Naibu Waziri Mkuu Barnaby Joyce, Seneta Fiona Nash, maseneta wa zamani wa chama cha Greens Scott Ludlam na Larissa Waters na Seneta wa chama cha One Nation Malcolm Roberts walipatwa kuwa ni raia wa nchi zingine, wakati waku wasilisha ombi lakuwania uchaguzi mkuu wa taifa wa 2016.

Seneta wa chama cha Nationals Matthew Canavan, aliye jiondoa katika baraza lamawaziri, na Seneta huru Nick Xenophon hawaku athiriwa kwa uamuzi wa mahakama kuu. Seneta Canavan ata endelea na majukumu yake kama Waziri wa Rasililimali na ukanda wa Kaskazini ya Australia.

Nafasi hizo tupu katika seneti sasa, zita amuliwa kupitia hesabu maalum ya kura zilizo pigwa katika uchaguzi wa 2016.

Wakati huo huo hatma ya Bw Joyce ita amuliwa kupitia uchaguzi mpya katika eneo bunge la New England tarehe 2 Disemba.


Share

1 min read

Published

By Rashida Yosufzai

Presented by SBS Swahili

Source: SBS World News




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service