Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Timu ya Taifa ya Iran itakuwa ya kwanza kuwasili Urusi kwa ajili ya Kombe la Dunia

Iran imepangwa kundi B wakiwa na mabingwa wa zamani Hispania, mabingwa wa Ulaya Ureno na Morocco.

Iran first team to arrive in Russia for World Cup

(Reuters) Source: Reuters

"Kuwa Urusi ni kama vile ndoto kuwa kweli kwa soka la Wairan.," Kocha wa Iran Carlos Queiroz alisema.

"Tumepata mafanikio haya kupitia kazi ngumu na kujitoa, kitu kilichoinua jinsi tunavyoheshimiwa na tunajisikia faraja kuwa hapa.

Iran itapiga kambi katika kituo cha mazoezi cha Lokomotiv Bakovka mjini Moscow. Hii itakuwa mara yao ya tano kuonekana kwenye fainali hizi za Kombe la Dunia.

Carlos Queiroz Iranian coach
Source: Getty

Queiroz alisikika akisema, "Iran itakuwa na kikosi kizuri, na tutahakikisha kuindeleza ndoto kwa muda mrefu iwezekanavyo na tunatarajia kucheza sehemu yetu katika kufanya hili Kombe la Dunia kuwa bora milele."

Timu hiyo ya Queiroz, inatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Lithuania mjini Moscow tarehe 8 mwezi huu wa sita na baadaye kuanza kampeini yao dhidi ya Morocco katika uwanja wa Mt Petersburg mnamo tarehe 15 mwezi huu.


1 min read

Published

Presented by Frank Mtao




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now