Polisi watoa video ya simu ya mwisho ya Justine Damond kwa 911

Sauti ya simu kutoka Justine Ruszczyk Damond kwenda kwa 99 inaonyesha, alikuwa anashindwa kupumua vizuri na inasikika alikuwa anaogopa sana wakati akitoa taarifa ya uwezekano wa kufanyiwa shambulizi nyumbani kwake Minneapolis.

Justine Damond Ruszczyk was shot dead by a police officer, after calling 911 about a possible sexual assault.

Justine Damond Ruszczyk was shot dead by a police officer, after calling 911 about a possible sexual assault. Source: AAP

Muhamasishaji wa itikadi za maisha ya Australia Justine Ruszczyk Damond alikuwa akipumua kwa tabu huku akipiga kelele wakati alpokuwa akipiga simu kwa namba ya dharura 911 kabla ya kupigwa risasi na polisi wa Marekani, kulingana na sauti ya simu.



Sauti mbili zilizorekodiwa za Bi Ruszczyk Damond kwenda kwa 911 zimeachiwa kwa umma Alhamis, wakati jaji wa Minneapolis alipoanza kuruhusu vizibiti kuonyeshwa katika kesi inayomuhusu Mohamed Noor.
Ex-police officer Mohamed Noor on May 1 before he was jailed over the fatal shooting of Justine Damond Ruszczyk .
Ex-police officer Mohamed Noor on May 1 before he was jailed over the fatal shooting of Justine Damond Ruszczyk . Source: AAP
Noor, mwenye umri wa miaka 33, alishtakiwa kwa mauji.
Justine Damond Ruszczyk was shot dead by a police officer, after calling 911 about a possible sexual assault.
Justine Damond Ruszczyk was shot dead by a police officer, after calling 911 about a possible sexual assault. Source: AAP
Bi Ruszczyk Damond, mwenye uraia pacha wa marekani na Australia, alipiga simu 911 kutoa taarifa juu ya uwezekano wa yeye kudhalilishwa kingono nyumbani kwakwe mnamo mwezi wa saba 2017.

Katika simu ya kwanza, alisema, alisikika mwanamke aliyeonekana kuteseka na anafikiria alisikia sauti ikiomba "msaada".

Bi Ruszczyk Damond alipiga tena dakika nane baadae ili kuhakikisha polisi walipata anuani sawa. Akataarifiwa kuwa, polisi wako njiani.

Mkazi huyo wa zamani wa Sydney akaenda kukutana na gari ya polisi ndipo akapigwa risasi na Noor, ambaye alikuwa amekaa kiti cha abiria cha mbele.
John Ruszczyk (left), the father of Justine Damond Ruszczyk, with his wife Marian Hefferen
John Ruszczyk (left), the father of Justine Damond Ruszczyk, with his wife Marian Hefferen. Source: AAP
Familia ya Bi Ruszczyk Damond walifungua mashtaka dhidi ya jiji la Minneapolis na wakafanikiwa kupewa kitita cha Dola za Kimarekani $US20 million sawa na Dola za australia ($A29 million) kama fidia.

 

 

 


Share

Published

By Frank Mtao
Presented by Frank Mtao

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service