Kamau na Tongyik wasajiliwa na Western Sydney Wanderers FC

Mashabiki wa Western Sydney Wanderers FC wame jawa kwa furaha baada yaku pokea taarifa kuwa wachezaji wa Melbourne City FC Bruce Kamau na Ruon Tongyik wame sajiliwa na Wanderers kwa miaka kadhaa.

Wachezaji wapya wa WSWanderers FC Bruce Kamau na Ruon Tongyik

Wachezaji wapya wa WSWanderers FC Bruce Kamau na Ruon Tongyik Source: Getty Images

Wawili hao hawaja pata fursa zaku tosha kucheza msimu huu kama ilivyo kuwa msimu ulio pita.

Bruce Kamau, 22, kwa mara nyingine atakuwa chini ya uongozi wa mkufunzi wa zamani wa Adelaide United na timu ya Australia ya wachezaji wa chini ya maika 23 Josep Gombau, ambaye chini ya uongozi wake, alikuwa mmoja wa nyota wakubwa wa soka katika A-League ambako alizua hisia mseto miongoni mwa walinzi alio kabiliana nao katika mechi. Image

Mchezo wa Kamau ulimfanya apendwe na mashabiki wengi wa Adelaide Utd, ambao aliwafurahisha zaidi, kwaku funga goli muhimu katika fainali ya A-League kabla ya kuhamia City mwaka wa 2016.

Josep Gombau pia alismsaidia Ruon Tongyik, 21, kuwa mlinzi mahiri ambaye huwa hasiti anapo kabiliana na washambuliaji wanao jaribu kuweka lango lake hatarini. Ruon alifaidi pia kupitia uongozi wa Gombau alipo chezea timu ya vijana wa Australia wenye umri wa miaka chini ya 23. Image

Bruce na Ruon wata kuwa wachezaji wa rasmi wa Wanderers mwisho wa msimu huu, ambako Gombau anaendelea na kazi yaku jenga upya timu aliyo rithi.


Share

1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano, SBS Swahili

Presented by SBS Swahili, Gode Migerano

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service