Kenya yaomboleza walio uawa katika shambulizi la ugaidi

Siku chache baada ya magaidi kushambulia hoteli laki fahari nama ofisi mjini Nairobi, Kenya taifa hilo la Afrika Mashariki, lina endelea kuhesabu gharama ya shambulizi hilo.

Wakenya washiriki katika mazishi ya walio uawa katika shambulizi lakigaidi katika hoteli ya DusitD2

Wakenya washiriki katika mazishi ya walio uawa katika shambulizi lakigaidi katika hoteli ya DusitD2 Source: AP

Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya Fred Matiang’i, alithibitisha taarifa ambazo wakazi wa taifa hilo, walikuwa wakisubiri kupitia taarifa aliyo toa kwa vyombo vya habari.

Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya Fred Matiang'i atoa taarifa kwa vyombo vya habari nje ya hoteli ya DusitD2
Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya Fred Matiang'i atoa taarifa kwa vyombo vya habari baada ya shambulizi laki gaidi katika hoteli ya DusitD2 mjini Nairobi,Kenya Source: AP
Taifa liko salama sasa na taifa lina endelea kuwa tulivu, wakenya na wageni wetu wote wako salama na wanastahili jihisi huru kuendelea kufanya shughuli zao kama kawaida. Tukumbuke sote kuwa, ugaidi hauta wahi tushinda, nasi kama taifa tuna endelea kuwa imara na hatuta jisalimisha wala kuogopa vitisho vya magaidi.

Imeripotiwa kuwa watu saba wamefariki, na mamlaka nchini humo wanatarajia idadi ya vifo kuongezeka uchunguzi unapo endelea baada ya shambulizi hilo la ugaidi. Ila familia zilizo fiwa, zime anza kuwazika wapendwa wao.

Wakenya washiriki katika mazishi ya walio uawa katika shambulizi lakigaidi katika hoteli ya DusitD2
Wakenya washiriki katika mazishi ya walio uawa katika shambulizi lakigaidi katika hoteli ya DusitD2 Source: AP
Wanamgambo wa al-Shabab kutoka Somalia, hawaku kawia kudai shambulizi hilo, wakidai shambulizi hilo lilisababishwa na hatua ya rais wa marekani Trump, kuhamishia ubalozi wake mjini Jerusalem.

Wakati huo huo inspekta mkuu wa polisi ya Kenya, Boinnet amewaomba wakenya waendelee kuwa watulivu na wasichangie picha zozote, kutoka shambulizi hilo uchunguzi unapo endelea.

 

 

 

 


Share

1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS Swahili




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service