Marudio ya uchaguzi wa urais yaendelea nchini Kenya licha ya upinzani kuususia

Wakenya wamerejea kwenye debe, katika marudio ya uchaguzi wa urais wa 26Oktoba 2017 ambao ume zua utata nchini humo.

Wakenya warejea katika marudio ya uchaguzi wa urais 26Oktoba2017

Wakenya warejea katika marudio ya uchaguzi wa urais 26Oktoba2017 Source: Andrew Kilonzi

Mamia ya vituo vyaku piga kura vilifunguliwa mapema, hata hivyo wapiga kura wengi hawaku jitokeza kupiga kura, hali ambayo wengi wanalinganisha na wapiga kura kusalimu amri ya mrengo wa upinzani ulio waomba wafuasi wake kususia uchaguzi huo.

Idadi ya walio shiriki katika ngome za chama tawala katika marudio ya uchaguzi huo, ilikuwa ndogo kulinganisha na idadi ya walio shiriki katika uchaguzi ulio pita.

Wakati huo huo tume ya uchaguzi ya IEBC imetangaza kuwa, maeneo yanayo aminika kuwa ngome za mrengo wa upinzani yata pewa fursa yakupiga kura kesho Jumamosi 28 Oktoba 2017, kwa sababu ya uharibifu na vizuizi vilivyo wekwa katika sehemu zakupigia kura kwa mujibu wa tangazo toka kwa Ubalozi wa Kenya nchini Australia.

Hata hivyo, Rais Uhuru Kenyatta kwa sasa anaongoza katika hesabu za marudio ya uchaguzi huo, wakati matokeo ya mwisho yanatarajiwa muda usio mrefu.

 


Share

1 min read

Published

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service