Ndege ya shirika la Lion Air yaanguka muda mfupi baada ya kupaa toka Jakarta

Ndege ya shirika la Lion Air imepata ajali hiyo leo Jumatatu, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kupaa toka Jakarta, Maafisa wa Indonesia walisema.

bango la taarifa za habari la SBS

bango la taarifa za habari la SBS Source: SBS News

Ndege hiyo ya Indonesian ya shirika la ndege la Lion imeanguka muda mfupi tu baada ya kuondoka mji mkuu wa Jakarta, maafisa wa masuala ya anga walithibitisha leo jumatatu huku wakiongeza kuwa, utafutaji na uokoaji unaendelea hivi sasa.

Ndege JT-610 iliondoka kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Soekarno-Hatta Jakarta saa 6.21asb Jumatatu na ilikuwa ikiongozwa na Pangkal Pinang.

Ndege ilipotea karibu na Karawang katika jimbo la West Java.

"Imethibitishwa kuwa imeanguka," Yusuf Latif, msemaji wa Shirika la Taifa la Utafutaji na Uokoaji, alisema kwa ujumbe wa maandishi.

Msemaji wa kampuni ya uongozaji safari AirNav aliliambia shirika la utangazaji la Metro kuwa, ndege hiyo Boeing 737-800 ilipotea kwenye mawasiliano ya redio.

Msemaji wa shirika hilo la Lion Air Danang Mandala Prihantoro alinukuliwa akisema: "Tunaweza kuthibitisha kuwa, moja ya ndege zetu zimepotea kwenye mawasiliano na sehemu ilipo, haijulikani kwa sasa."

Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje aliliambia shirika la habari la SBS kuwa, itatutaarifu kama kuna Muastralia yoyote aliyeathirika kwa ajali hiyo.


Share

1 min read

Published

Updated

By Frank Mtao

Presented by Frank Mtao




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service