'Sauti kubwa ilirindima': Mashahidi wanasema kwamba ndege ya Ethiopia ilionekana ikitoa moshi

Mashahidi waliokuwa mashamabni ambako Ndege ya Ethiopia ilianguka wamesema waliona moshi mkubwa wakati wengine wanne wakielezea kusikia mlio mkubwa wa sauti.

Rescue workers carry wreckage at the crash site of Ethiopia Airlines Boeing 737 Max 8 en route to Nairobi, Kenya, near Bishoftu, Ethiopia.

Rescue workers carry wreckage at the crash site of Ethiopia Airlines Boeing 737 Max 8 en route to Nairobi, Kenya, near Bishoftu, Ethiopia. Source: AAP

Ndege ya shirika la ndege la Ethiopia ambayo ilianguka na kuua watu 157, ilikuwa ikitoa kelele ya ajabu huku ikifuatiwa na moshi mzito pamoja na mabaki yakimeguka ikiwa angani juu ya shamba la ng'ombe waliogopa, kabla ya kupiga ardhi, kulingana na mashahidi.

Ndege hiyo namba 302 iliondoka mji mkuu wa Ethiopia siku ya Jumapili asubuhi ikielekea Nairobi ikiwa na abiria kutoka nchi zaidi ya 30.

Wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo Boeing 737 MAX-8 walifariki.

Rubani wa ndege hiyo, aliomba ruhusa ya kurudi, akisema alikuwa na matatizo - lakini ilikuwa tayari amechelewa.

Nusu ya mashahidi kadhaa waliohojiwa na Reuters katika mashamba ambapo ndege ilipoangukia, walisema, waliona moshi mzito, huku wanne wao walielezea kusikia mlio wa sauti kubwa.

"Ilikuwa ni mlio wa sauti ya kelele." Kama muanguko wa vyuma, alisema Turn Buzuna, mama wa nyumbani mwenye umri wa miaka 26 na mkulima ambaye anaishi mita 300 kutoka sehemu ndege hiyo ilipoangukia.

"Kila mtu anasema hawajawahi kusikia aina hiyo ya sauti kutoka kwenye ndege na ambayo iko chini ya njia yake."

Malka Galato, mkulima wa shayiri na ngano ambaye shamba lake ndipo ndege iliangukia ndani, pia alieleza kuona moshi na cheche nyuma ya ndege hiyo.

"Ndege ilikuwa karibu sana na ardhi na ikazunguka... Ng'ombe ambazo zilikuwa zinapata malisho shambani zilikimbia," alisema.
Photographs of the crew members of the Ethiopian Airlines flight ET 302 that crashed are displayed during a memorial service.
Photographs of the crew members of the Ethiopian Airlines flight ET 302 that crashed are displayed during a memorial service. Source: AAP
Tamirat Abera, mwenye umri wa miaka 25, alikuwa akitembea kwenye shamba wakati ule.

"Kulikuwa na moto na moshi mweupe ambao baadaye ukageuka mweusi," alisema

"Wakati ilipokuwa ikihaha angani, moto ulikuwa ukifuata mkia wake, kisha ikajaribu kuinua pua yake kupaa," mwingine Shahidi Gadisa Benti alisema.

"Baada ya kupita juu ya nyumba yetu, pua ilielekea chini na mkia uliinuka, ikaenda kupiga chini pua yake, kisha ikalipuka."

Mwezi Oktoba uliopita, muundo sawa wa ndege, unaoendeshwa na shirika la ndege la Lion, ilipata ajali nchini Indonesia, na kuua watu 189.

Uchina - ambao ni soko muhimu kwa Boeing - ikawa nchi ya kwanza kusimamisha ufanyaji kazi ndege hizo aina ya  737 MAX-8 siku ya Jumatatu. Ndege za Ethiopia zilifanya hivyo, wakisema uamuzi ulikuja kama "tahadhari ya ziada ya usalama."


Share

2 min read

Published

By Frank Mtao

Source: SBS




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service