Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Lucy Gichuhi:"Mimi ni raia wa Australia, na niko tayari kutoa huduma"

Lucy Gichuhi ni mwanasheria na ni mzawa wa Kenya. Ame chaguliwa kuwakilisha jimbo la Kusini Australia ndani ya bunge la shirikisho, baada ya mahakama kuu kuamua uchaguzi wa kiongozi wa chama cha Family First Bob Day katika Seneti ulikuwa batili.

Seneta wa Kusini Australia, Lucy Gichuhi
Seneta wa Kusini Australia, Lucy Gichuhi Source: AAP
Bi Gichuhi amechapisha tangazo akisema:
"Hesabu ya kura imethibitisha kwamba, mimi Lucy Gichuhi, nime chaguliwa kuwakilisha Kusini Australia ndani ya Seneti ya Australia".

Hesabu hiyo maalum ilifanywa na tume ya uchaguzi ya Australia Alhamisi mjini Adelaide.

"Nina heshima na shukrani kwa fursa yaku wahudumia wana Australia. Hii ni fursa yakutoa mchango wangu kwa taifa hili". "Sita zungumzia mchakato ambao umetufikisha hapa. Kama mwanasheria, nina heshimu mchakato waki sheria na uchaguzi" alisema. "Mimi ni raia wa Australia na nime fuzu kutoa huduma. Nita endelea kupokea ushauri kwa maswala haya yote tunapo endelea mbele.”

Hata hivyo chama cha Australian Labor (ALP) kime pinga uraia wake, swala hilo lita rejea katika mahakama kuu wiki ijayo, ambako uamuzi wa mwisho utatolewa kwa atakaye chukua nafasi ya Bw Day.


1 min read

Published

Updated

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS




Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now