Aliyepanda daraja la Sydney Harbour bila kibali, ajisalimisha kwa Polisi.

Mwanaume huyo aliyepanda daraja hilo na kusababisha patashika kubwa na Polisi kwa zaidi ya masaa matano, ameshushwa chini na kutiwa pingu na maafisa usalama.

Drama la Sydney Harbour

Picha ya maktaba Source: SBS

Mtu huyo mwenye umri wa takribani miaka 40 hivi, aliyekuwa amevalia vazi aina ya 'tracksuit', kofia na glavu za mikononi zilizoacha vidole vyake wazi, alipanda daraja hilo majira ya saa 10:30 alfajiri ya leo hii Jumatano.

Ila baada ya saa 3:30 asubuhi, alijisalimisha kwa wana usalama na akashuka toka juu kuelekea kilipo kikosi cha uokoaji cha Polisi ambao walimfunga pingu na kumshusha chini.

"Tunaweza kuthibitisha kuwa, mtu huyo yuko salama chini ya ulinzi wa Polisi," Polisi NSW ilisema kupitia mtandao wa tweeter.

Aliwekwa kwenye machela na kuchukuliwa na gari ya wagonjwa ya kikosi cha huduma ya kwanza.

Foleni za magari zilikithiri wakati wa tukio hilo, kwani iliwapasa maafisa usalama kufunga baadhi ya barabara wakati wakiwa wanafanya mazungumzo na mtu huyo. 

Ilipofika mida ya saa 2 asubuhi, foleni ya magari kupita darajani hapo ilikuwa kubwa kwa zaidi ya kilomita 15 kwa pande zote mbili hasa file za kuingia mjini.

Mabasi kupita darajani hapo, yalicheleweshwa kwa zaidi ya nusu saa lakini treni zilikuwa zikipita kama kawaida.

Si ruhusa kupanda daraja la Sydney Harbour isipokuwa kwa kibali maalumu na anayekamatwa kwa tukio hilo, anaweza kupigwa faini $3000. 


Share

2 min read

Published

Updated

By AAP-SBS

Presented by Frank Mtao

Source: AAP, SBS



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service