Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Mbappe akosa kufanya mazoezi na timu yake ya taifa ya Ufaransa ikiwa ni masaa machache tu kabla ya nusu fainali kombe la dunia

Mshambuliaji huyo wa Ufaransa, hakushiriki mazoezi hayo usiku kuamkia nusu fainali ya kombe la Dunia la FIFA 2018 dhidi ya Ubelgiji.

Mbappe

(Getty Images) Source: Getty

Kijana toka timu ya Paris Saint-Germain, Mbappe, amekuwa nyota katika michuano hiyo ya Urusi, akifunga mara tatu, ukijumuisha umahiri aliouonyesha dhidi ya Argentina kwenye mzunguko wa 16.

Kocha mkuu Didier Deschamps aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano kabla ya mazoezi hayo kuwa, anatarajia kuwa na kikosi chake kamili kukabiliana na vijana wa Roberto Martinez na akafafanua kuwa, wachezaji wamepumzishwa mazoezi hayo kama tahadhari.

Ngolo Kante
(Getty Images) Source: Getty

Pia wakati wa kuanza mazoezi hayo katika uwanja wa Krestovsky, Benjamin Pavard na N'Golo Kante walikuwa wakifanya mazoezi pembeni ya kikosi wakiwa wanakimbia taratibu kuzunguka uwanja chini ya usimamizi wa makocha wengine wa timu hiyo ya Ufaransa.

Nusu fainali za michuano hiyo ya Dunia inatarajia kuanza kuunguruma alfajiri hii kwa saa za hapa Australia pale Ufaransa itakapokabiliana na Ubelgiji na nusu fainali ingine kuchezwa keshokutwa alfajiri ambapo Uingereza itamenyana na Kroatia.

Michezo yote hii itaonyesha na runinga yako ya SBS moja kwa moja kutoka Urusi.


1 min read

Published

Updated

By sbs

Presented by Frank Mtao

Source: Omnisport and SBS The World Game



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now