Wanamichezo wengine zaidi wa Afrika watoroka

Wanamichezo wa Jumuiya za madola wameonywa kuwa, hatua kali zitachukuliwa iwapo watavunja sheria za viza zao, hii inatokana na Waafrika kadhaa kutoonekana michezoni.

Commonwealth Games

Matam Matam Olivier Heracles of Cameroon competes during the Weightlifting Men's 62kg Final at the Commonwealth Games Source: Getty images

Timu ya wanaume ya mchezo wa 'squash' kutoka Sierra Leone na mkufunzi wa wanyanyua vyuma toka Rwanda, wamo miongoni mwa Waafrika wanamichezo walitoweka katika michuano ya Jumuiya za Madola mjini Gold Coast.

Hii inakuja ndani ya masaa machache yaliyopita baada ya Waziri wa mambo ya ndani Peter Dutton kuwaonya wanariadha watakaovunja sheria juu ya vibali vyao vya kusafiria kuwa watatafutwa na kukamatwa kisha kurudishwa nchi zao.

Wanamichezo Ernest Jombla na Yusif Mansaray kutoka Sierra Leone, hawakuonekana kwenye mchezo wao wa pamoja leo Alhamis asubuhi.

Hii ina maana, Jombla na Mansaray walishindwa kuhudhuria michezo yao mjini Gold Coast baada ya kutoonekana siku ya Jumanne kwa mchezo dhidi ya Peter Creed na Joel Makin kutoka Wales.

Licha ya wawili hao kutoonekana katika michezo yao, Maafisa wa Sierra Leone walisisitiza kuwa, wawili hao walikuwa bado kwenye kijiji hicho cha michezo ila walichanganyikiwa na mida ya michuano yao.
File image of Cameroon's Simplice Fotsala
Cameroon's Simplice Fotsala Source: AAP
Naye afisa mwandamizi wa Rwanda, Eugene Nzabanterura amesema, mkufunzi wao Jean Paul Nsengiyuma hajaonekana tangu kumalizika kwa mchezo wake katika kiwanja cha Carrara Sports siku ya Jumanne.

Taarifa zingine zilitolewa kuhusiana na kutoonekana kwa wanamichezo wengine Waganda wawili , lakini maafisa wa timu yao walidai wanamichezo wao na viongozi wote wapo.

Taarifa hizi zinakuja siku moja baada ya wanamichezo wanane kati ya 42 wa Cameroon kutoweka, ikijumuishwa mabondia wawili ambao hakauonekana kwenye mapambano yao.
Gold Coast 2018 Commonwealth Games
Minkoumba Petit David of Cameroon competes during Men's 94kg final of Weightlifting on day four of the Gold Coast 2018 Commonwealth Games Source: Getty Images
Wanariadha wengi wako kwenye viza zinazowaruhusu kukaa nchini hadi tarehe 15 mwezi wa Tano lakini Dutton alitilia mashaka kutokuonekana kwa wanamichezo hao kwenye michezo ya mashindano yao ikiwa hayo ndiyo yaliyowaleta.

 Mkuu wa michezo ya Jumuiya za madola Peter Beattie alisema, ingawaje vibali vya kusafiria wanamichezo hao vinawaruhusu kutembea popote na kufurahia Australia, ila wanatakiwa kurudi nchi zao kama ilivyopangwa.


Share

2 min read

Published

Presented by Frank Mtao

Source: AAP



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service