Shirikisho la chama chaKiislamu nchini Burkina Faso limelaani shambulio baya la Kigaidi lilofanywa na wanamgambo wa Kiislamu wenye msimamo mkali nchini humo.
Majeruhi katika tukio hilo, lilotokea katika hotel ya kisasa mjini Ouagadougou, amesema wanamgambo hao walikuwa wakiwalenga wazungu.
Vikosi vya Usalama vikiongozwa na jeshi la Ufaransa na Marekani, vilisaidia kuirudisha hotel katika himaya ya usalama baada ya masaa kadhaa ya operetaion hiyo ambapo wanamgambo wanne waliofanya mashambulizi hayo waliuawa papo hapo.
Wakati mateka 150 wakiachiliwa huru, takribani watu 23 kutoka mataifa 18 walifariki dunia katika shambulio hilo , huku mmoja wa waliojeruhiwa akisema wanajihadi hao walirudi mara kwa mara katika hoteli hiyo maarufu kwa watalii ili kuwapiga tena risasi majeruhi waliokuwa wamelala chini kwa kunyanyua meza na viti.
Sheikh Sidi Mohamed Saday kutoka shirikisho la Burkina Faso chama cha Kiislamu alisema, shambulio hilo linahitaji kukemewa.
Alisema, "Kama raia wa Burkina Faso, na vile vile Muislamu - tumehudhunishwa sana na mashanbulizi haya. Baadhi ya watu wameliteka jina la Kiislamu. Hatuutambui Uislamu katika matendo haya. Tunalaani ushenzi huu. Haiwezi kuelezewa na dini yoyote."

