NASA: Raila Odinga ndiye Rais wa 5 wa Kenya

Wakenya wana endelea kusubiri tangazo rasmi la atakaye kuwa rais wa 5 wa taifa hilo kutoka IEBC, hata hivyo mmoja wa vinara wa chama cha muungano cha NASA Musalia Mudavadi ametoa tangazo kwa vyombo vya habari akiwaeleza viongozi wa IEBC, wamtangaze kiongozi wao Raila Odinga kuwa ndiye mshindi wa uchaguzi wa urais.

Kinara wa muungano wa NASA Musalia Mudavadi akizungumza na vyombo vya habari

Kinara wa muungano wa NASA Musalia Mudavadi akizungumza na vyombo vya habari mjin Nairobi, Kenya, 10 Agosti 2017. Source: EPA/Kabir Dhanji

Bw Mudavadi alieleza vyombo vya habari kupitia tangazo hilo kuhusu hitilafu nyingi, zinazo husiana na matokeo ya uchaguzi yaliyo kuwa yaki tangazwa na IEBC kwa upande wa uchaguzi wa urais.
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari Source: NASA Kenya
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari Source: NASA Kenya
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari
Taarifa ya chama cha muungano wa NASA kwa vyombo vya habari Source: NASA Kenya
Akizungumza kwa niaba ya muungano wa NASA, Bw Mudavadi amedai chama chake kime pokea matokea halisi ya uchaguzi wa urais kutoka mtu mmoja ndani ya tume la IEBC. Matokeo hayo yame baini kuwa kinara wa NASA Bw Raila Odinga ana kura nyingi zaidi ya mpinzani wake Bw Uhuru Kenyatta.
Bw Mudavadi, ameleza tume ya IEBC itangaze rasmi Bw Odinga kuwa ndiye mshindi wa uchaguzi wa urais wa 2017. Kwa mujibu wa Bw Mudavadi, hesabu halisi za kura za urais ndani ya mitambo ya IEBC, zime mpa Bw Raila Odinga kura 8,056,885 ilhali Bw Uhuru Kenyatta ana kura 6,659, 493.
Hata hivyo, tume ya IEBC ime sisitza uhuru wayo na kwamba, ita tangaza matokeo rasmi itakapo kuwa tayari.

 


Share

Published

Updated

By SBS Swahili
Presented by SBS Swahili
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
NASA: Raila Odinga ndiye Rais wa 5 wa Kenya | SBS Swahili