Wanafunzi 9 wauawa kwa shambulio la kisu nchini China

Wanafunzi tisa, wameua na wengine 10 kujeruhiwa katika shambulio la kisu shuleni, Kaskazini ya China.

File

Source: AAP

Mtu mmoja mwenye kisu, amewaua watoto tisa wa shule za msingi na kujeruhi wengine 10 wakati wakiwa wanarudi majumbani huko Kaskazini China siku ya ijumaa, maafisa walisema, ni tukio kubwa la kutisha kutokea katika miaka ya hivi karibuni.

Mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 28 alikamatwa na watoto waliojeruhiwa walikuwa wakipatiwa matibabu, alisema afisa wa usalama wa umma eneo la Mizhi kupitia mtandao wa kijamii.

Wasichana saba na vijana wa kiume wawili waliua katika tukio hilo, kwa mujibu wa shirika la habari la Xinhua, wakiwanukuu polisi wa eneo hilo. Umri wa watoto haukutajwa, lakini umri wa wanafunzi wa shule ya msingi inakadiriwa kuwa ni kati ya 12 na 15 nchini China.

Kwa mujibu wa maafisa usalama wa umma walisema, mtu huyo aliyejulikana kwa jina la Zhao kutoka kijiji cha  Zhaojiashan kitongoji cha  Mizhi alikamatwa.

Walisema, mtuhumiwa alikiri kuwa, alikuwa akidhihakiwa na kuzomewa wakati akiwa anasoma darasa la tatu akiwa mdogo, hivyo aliwachukia wana darasa wenzake na kuamua kutumia kisu chenye ncha kali kuwaua watu siku ya Ijumaa.

 





Share

1 min read

Published

Updated

By AAP-SBS

Presented by Frank Mtao

Source: AAP, SBS



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service