Maofisa wa Ubalozi wafukuzwa kazi kwa tuhuma za ubadhilifu wa masuala ya ’VIZA'

Maofisa wawili wa Ubalozi wa Australia nchini Afrika ya Kusini, wamefukuzwa kazi kufuatia uchunguzi juu ya kashfa ya kuchukua rushwa kutoa viza kwa watu.

An Australian passport is pictured next to an entry visa to Papua New Guinea in Brisbane.

File photo Source: AAP

Maofisa hao, wanahusishwa na kuchukua hongo kutoka kwa raia wa Naijeria ili kuwapa vibali vya kuishi.

Gazeti la The Herald Sun limetoa taarifa kuwa, takribani raia 21 wa Naijeria, walipata viza za Australia za uanafunzi ambapo uchunguzi wa hali wa kina ulibaini, maofisa wala rushwa wanidara hiyo ndio walifanikisha zoezi hilo.
imagejpeg
Gazeti hilo liliendelea kubainisha kuwa, Idara ya mambo ya ndani ilithibitisha kuwa, raia wawili wasio Waustralia, wanaofanya kazi Ubalozi wa Australia nchini Afrika Kusini wamefukuzwa kazi.

Maofisa hao wanatuhumiwa kuwapa visa watu wanaoshukiwa kuwa hatari Australia pasipo kupitia hatua muhimu za uangalizi wa maombi.
imagejpeg
Viza hizo 21, zilipitishwa mnamo mwezi wa pili hadi wa nne mwaka jana, kwa mujibu wa hati ya rufaa ya mahakama.

Hati hiyo inasomeka kuwa, viza hizo zilitambulika kupitishwa kupitia rushwa kutoka kwa maofisa wa idara hiyo.


Share

1 min read

Published

Presented by Frank Mtao



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service