Paul Kagame awafagia wapinzani wake

Rais mteule Paul Kagame, ame washukuru raia wa Rwanda walio nje na ndani ya nchi kwa kumchagua tena kuongoza taifa hilo.

Paul Kagame kwenye kampeni ya uraisi Rwanda

Paul Kagame kwenye kampeni ya uraisi Rwanda Source: Paul Kagame

Taarifa kutoka tume ya uchaguzi nchini Rwanda, zinasema kwamba Paul Kagame ameshinda uchaguzi mkuu wa uraisi kwa 98.63% ya kura. Mpinzani wake wa karibu Philippe Mpayimana alipata 0.73% ya kura naye Frank Habineza alipata 0.47 ya kura.

Matokeo ya kura ya urais Rwanda
Matokeo ya kura ya urais Rwanda Source: NEC Rwanda
Rais Kagame na familia yake walijiunga na mamia yama elfu ya raia wa Rwanda, katika vituo vyaku piga kura, kuamua atakaye ongoza taifa hilo kwa miaka saba ijayo.

Wanyarwanda wanao ishi Australia, nao pia walishiriki katika uchaguzi huo.

Rais Kagame aweka kidole wino kabla ya kupiga kura
Rais Kagame aweka kidole wino kabla ya kupiga kura Source: Paul Kagame

Rais Kagame amekuwa madarakani kwa miaka kumi na saba, na sasa atahudumu muhula wa tatu wa miaka saba. Katiba ya Rwanda ilifanyiwa mabadiliko mwaka 2015, na kumpa Rais Kagame fursa ya kusalia madarakani hadi mwaka 2034.

Wafuasi wake wanamsifu kwa kuleta utulivu na maendeleo ya kiuchumi nchini humo baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 ambapo mamia yamaelfu ya watu waliuaawa.

 


Share

1 min read

Published

Updated

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service