Breaking

Raila apoteza kura ya uenyekiti wa AU

Viongozi wa mataifa ya Afrika wali tua mjini Addis Ababa, Jumamosi 15 Februari 2025 kumchagua kiongozi mpya wa Muungano wa Afrika (AU).

Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Mh Raila A Odinga

Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Mh Raila A Odinga Credit: Raila A Odinga

Viongozi hao walikuwa na jukumu la kuchagua kati ya Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nje wa Madagascar Richard Randriamandrato, na Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, Mahmoud Ali Youssouf.

Matarajio ya Raila Odinga kushinda wadhifa huo yalipokea pigo kupitia barua ya katibu mkuu wa SADC, iliyo tangaza kuwa nchi wanachama wa muungano huo watampigia kura mwanachama wao kutoka Madagascar, Richard Randriamandrato.

Tangazo hilo lili maanisha Bw na Raila na Bw Mahmoud, walikuwa wamepoteza kura walizo tarajia kutoka wanachama wa SADC.

Baada ya raundi kadhaa za kura, Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, Mahmoud Ali Youssouf ili ibuka mshinidi wa uchaguzi huo na ata hudumu kwa miaka minne ijayo.

Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Raila apoteza kura ya uenyekiti wa AU | SBS Swahili