Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

NASA: Raila tosha

Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya wa National Super Alliance (NASA), umemteua waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, kuwa mgombea wake wa kiti cha urais kwenye uchaguzi ujao wa mwezi Agosti.

Mh Raila A Odinga, mgombea wa NASA 2017
Mh Raila A Odinga, mgombea wa NASA 2017 Source: Raila A Odinga

Makamu wa rais wa zamani Kalonzo Musyoka, ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Wiper Democratic Movement, ameteuliwa kuwa mgombea mwenza wa bwana Odinga.

Image

Bwana Odinga sasa atakabiliana na Rais Uhuru Kenyatta, atakayetumia chama cha Jubilee kuwania muhula wa pili.

"Hii ni heshima kubwa sana ambayo ndugu zangu wamenifanyia, kwa kuniweka nipeperushe bendera ya NASA. Tumekuwa na vikao ambavyo vimechukua siku nyingi. Kila kitu tumeandika.”

Bwana Odinga alisema wakati akihutubu baada ya kutangazwa kuwa mgombea wa NASA.

Kikosi hicho cha NASA kilitangazwa jana Alhamisi kwenye mkutano mkubwa wa hadhara ulioandaliwa katika bustani ya Uhuru mjini Nairobi.

Viongozi wa chama cha mseto cha NASA
Viongozi wa chama cha mseto cha NASA Source: Raila A Odinga
Wanachama wengine wakuu watatu wa muungano wa NASA Musalia Mudavadi, Moses Wetangula na Isaac Ruto, nao wamepewa nyadhifa za juu katika muungano huo, ambazo watatekeleza ikiwa watashinda urais kwenye uchaguzi wa Agosti.

Ikiwa watashinda, waziri mkuu mratibu wa shughuli za serikali atakuwa kiongozi wa chama cha Amani National Congress Musalia Mudavadi.

Bango la chama cha Mh Musalia Mudavadi
Bango la chama cha Mh Musalia Mudavadi Source: Musalia Mudavadi

Naibu waziri mkuu mratibu wa uchumi atakuwa kiongozi wa Ford Kenya Moses Wetangula.

Image

Kiongozi wa Chama cha Mashinani (CCM) Isaac Ruto atakuwa naibu waziri mkuu atakayesimamia utawala na huduma za jamii.

Image


1 min read

Published

Updated

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now