Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Rigathi Gachagua achaguliwa kuwa mgombea mwenza wa William Ruto

Siku moja kabla ya tarehe ya mwisho yakuwasilisha jina la mgombea mwenza wa urais katika uchaguzi mkuu wa Kenya, Dkt William Samoei Ruto amemtangaza Rigathi Gachagua kuwa mgombea wake mwenza wa mrengo wa Kenya Kwanza.

Mgombea wa Urais wa Kenya William S Ruto (kulia) na mgombea wake mwenza Rigathi Gachagua (kushoto)
Mgombea wa Urais wa Kenya William S Ruto (kulia) na mgombea wake mwenza Rigathi Gachagua (kushoto) Source: William S Ruto

Joto la siasa nchini Kenya limekuwa likiongezea kila siku, na mrengo wa Kenya Kwanza uliteka fikra na hisia za taifa hilo kwa masaa kadhaa, mgombea wao Naibu Rais William S Ruto aliposoma hotuba ndefu na hatimae akamtangaza mgombea wake mwenza Rigathe Gachagua.

Prof Kindiki katika kampeni ya UDA
Prof Kindiki katika kampeni ya UDA Source: Kithure Kindiki
Bw Gachagua alikuwa akiwania wadhifa huo dhidi ya mwanasheria wa Bw Ruto, Prof Kithure Kindiki. Imeripotiwa kuwa sikumoja kabla, wawili hao walishiriki katika mazungumzo magumu yakujaribu kutatua swala la atakaye mgombea mwenza wa Bw Ruto bila mafanikio.

Hata hivyo, Bw Gachagua ame ibuka mshindi wa kinyang'anyiro hicho cha mgombea mwenza. SBS itakuletea maelezo zaidi kuhusu uteuzi huo punde tutakapo pata taarifa zaidi.

 

 


1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS Swahili


Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now