Rigathi Gachagua achaguliwa kuwa mgombea mwenza wa William Ruto

Siku moja kabla ya tarehe ya mwisho yakuwasilisha jina la mgombea mwenza wa urais katika uchaguzi mkuu wa Kenya, Dkt William Samoei Ruto amemtangaza Rigathi Gachagua kuwa mgombea wake mwenza wa mrengo wa Kenya Kwanza.

Mgombea wa Urais wa Kenya William S Ruto (kulia) na mgombea wake mwenza Rigathi Gachagua (kushoto)

Mgombea wa Urais wa Kenya William S Ruto (kulia) na mgombea wake mwenza Rigathi Gachagua (kushoto) Source: William S Ruto

Joto la siasa nchini Kenya limekuwa likiongezea kila siku, na mrengo wa Kenya Kwanza uliteka fikra na hisia za taifa hilo kwa masaa kadhaa, mgombea wao Naibu Rais William S Ruto aliposoma hotuba ndefu na hatimae akamtangaza mgombea wake mwenza Rigathe Gachagua.

Prof Kindiki katika kampeni ya UDA
Prof Kindiki katika kampeni ya UDA Source: Kithure Kindiki
Bw Gachagua alikuwa akiwania wadhifa huo dhidi ya mwanasheria wa Bw Ruto, Prof Kithure Kindiki. Imeripotiwa kuwa sikumoja kabla, wawili hao walishiriki katika mazungumzo magumu yakujaribu kutatua swala la atakaye mgombea mwenza wa Bw Ruto bila mafanikio.

Hata hivyo, Bw Gachagua ame ibuka mshindi wa kinyang'anyiro hicho cha mgombea mwenza. SBS itakuletea maelezo zaidi kuhusu uteuzi huo punde tutakapo pata taarifa zaidi.

 

 


Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Rigathi Gachagua achaguliwa kuwa mgombea mwenza wa William Ruto | SBS Swahili