Kwa miezi kadhaa chama cha Raila Odinga, ODM kili sisitiza kuwa hakiko serikalini wala hakina ushirikiano wowote na serikali ya Dkt Rutto.

Madai hayo yali tolewa licha ya chama hicho kuwapa baraka viongozi wake wanne kuwa mawaziri katika serikali ya Kenya Kwanza.
Rais Rutto na Bw Odinga waliwasili katika ukumbi wa KICC, kutia saini makubaliano ya ushirikiano kati ya serikali ya Kenya Kwanza na chama cha upinzani cha ODM.

Tukio hilo limepokewa kwa hisia mseto katika taifa hilo la Afrika Mashariki, wachambuzi na raia wakijumuika katika mitandao yakijamii kuchangia maoni yao.

