SBS Swahili ilihudhuria sherehe iliyo andaliwa na shirika la Celebrate African Australians NSW ndani ya ukumbi wa Canada Bay Club, katika kitongoji cha Five Dock, NSW.
Shirika hilo hupokea pendekezo kutoka wanachama wa jumuiya zawana Afrika wanao ishi Australia, kwa ajili yakuwatambua watu ndani ya jamii wanao toa mchango chanya katika jami.
SBS Swahili ilipendekezwa kupokea tuzo mwaka huu kwa huduma inayo toa katika jamii, tunawashukuru wote walio tupendekeza kupokea tuzo hii kwa huduma tunayo toa katika jamii kupitia vyombo vya habari.

Shukran tena kwa kila mtu aliye tupendekeza kupokea tuzi hii, na asante pia kwa wasikilizaji wetu wote kwakuendelea kutu unga mkono. Tuna tumai tuta endelea kushirikiana pia katika mwaka wa 2017.
Share

