Scott Morrison apunguza pengo la kupigiwa kura na Labor kabla ya mjadala wa kwanza wa viongozi

Serikali ya Umoja sasa imepunguza kiasi chake hadi asilimia moja nyuma ya chama cha Labor katika matokeo ya kura za maoni za hivi karibuni.

Bill Shorten and Scott Morrison will have a leaders' debate in Perth on Monday night.

Bill Shorten and Scott Morrison will have a leaders' debate in Perth on Monday night. Source: AAP

Waziri Mkuu Scott Morrison na Kiongozi kambi ya upinzani wanajiandaa kukabiliana na mjadala muhimu kama kura za maoni za hivi karibuni zinaonyesha Serikali ya Umoja huo inapata unafuu.

Kura za maoni hizo zilizochapishwa na gazeti The Australian siku ya Jumapili usiku, zimeonyesha serikali iko na asilimia moja tu nyuma ya Upinzani katika maoni ya chama kipi kipewe kipaumbele baada ya kuanza kwa nguvu kwa kipindi cha wiki tano za kampeni.

Bwana Morrison anaingia katika mjadala kwa kasi huku wengi wakibashiri kuboreshwa katika uchaguzi kutokana na  utendaji wake wenye nguvu katika kampeni za uchaguzi.

Bwana Morrison ametilia mkazo shambulizi lake kwa Upinzani ambapo amekejeli mipango ya kodi ya chama cha Labor na kumshambulia Bill Shorten kwa kumuita "dubu mwenye hasira". 

Lakini, kura za awali zinaonyesha serikali ya Umoja imeshuka asilimia moja hadi kufikia asilimia 38, wakati chama cha Labor kiko chini kwa asilimia 37


Share

Published

By Rosemary Bolger
Presented by Frank Mtao
Source: SBS News

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service