Licha ya kuongezeka muda huo wa kutafuta katika kina kirefu chini ya bahari eneo la Point Lonsdale, bado mabaki ya ndege hiyo kwa jina la Piper Cherokee iliyoanguka baharini siku ya ijumaa hayajapatikana.
Miili ya watu watatu ilipatikana masaa machache tu baada ya ajali hiyo lakini mwili wa mtu wa nne haujapatikana.
Polisi wamesema, huenda ikawa mwili huo umejifunga ndani ya mabaki ya ndege hiyo takribani mita 30 chini ya usawa wa bahari katika eneo la utafutaji la ukubwa wa mita 500.

