Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Serena Williams anusurika mtihani wake mgumu wa mapema

Bingwa mtetezi na namba moja kwa ubora duniani, Serena Williams amenusurika mtihani wake mgumu wa mapema kuendelea na mzunguko wa pili wa michuano ya tenisi ya wazi ya Australia yanayofanyika mjini Melbourne.

Serena Williams wa Marekani akishangilia baada ya kumchapa Camila Giorgi wa Italy katika mchezo wa mzunguko wa kwanzamichuano ya tenis maarufu 'Australian Open' mjini Melbourne, Australia, Jumatatu, Jan. 18, 2016.(AP Photo/Vincent Thian)
Serena Williams of the United States celebrates after beating Camila Giorgi of Italy during their first round match at the Australian Open tennis championships in Melbourne, Australia, Monday, Jan. 18, 2016.(AP Photo/Vincent Thian) Source: AP

Bingwa mara sita, alihitaji saa moja na dakika 45 kumchakaza Muitaliano Camila Giorgi kwa alama 6-4 7-5 katika hali ya hewa ya joto kali siku ya kwanza ya michuano hiyo.

Kuumia kwa goti kumlizuia Williams kushiriki mashindano tangu yale ya wazi ya Marekani mnamo mwezi wa tisa, lakini Muamerika huyu alikuja bila kujeruhiwa kupata tiketi yake ya mzunguko wa pili utakaochezwa siku ya jumatano ambapo atakutana na kati ya Mlatvia,  Jelena Ostapenko au Mtaiwani, Su-Wei Hsieh.

Williams aliliambia runinga ya Channel Seven kuwa, aliridhishwa kwa kupewa mtihani huo mzuri katika mchezo wake wa kwanza kwenye michuano hiyo maarufu kama 'Australian Open'.

Alisema, "Yeah, haikuwa rahisi. Bila shaka alicheza vizuri sana na anajua kuupiga vyema mpira. Na sijacheza mchezo wowote wa mashindano kwa muda mrefu sana, lakini nafikiri ilikuwa vizuri kwangu kuja hapa na kufanikiwa kuendelea mbele. Na haikuwa haraka, na hilo kwa kweli lilikuwa kwa manufaa yangu pia."


1 min read

Published

Updated

By Frank Mtao

Source: SBS News



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now