Shujaa wa ahidi matokeo mazuri zaidi, katika mechi zinazo salia za mzunguko wa 7s

Mamia yawa Kenya kutoka mikoa tofauti ya Australia, walijumuika katika eneo la michezo ya olimpiki mjini Sydney, kushuhudia michuano ya kila mwaka ya raga ya Sydney7s.

Jacob Ojee Nahodha wa Shujaa Kenya

Jacob Ojee Nahodha wa timu ya taifa ya Kenya ya raga, ya wachezaji saba, mjini Sydney baada ya kushiriki katika michuano ya Sydney 7s 2019 Source: SBS Swahili

Mashabiki wa Shujaa (Kenya) wali wasili katika michuano ya Sydney7s wakiwa na matumaini yaku shuhudia nchi yao ikishinda moja ya kombe zilizo kuwa zikiwaniwa.

Mashabiki wa shujaa, katika michuano ya Sydney 7s 2019
Mashabiki wa shujaa, katika michuano ya Sydney7s 2019 Source: SBS Swahili
Matarajio hayo yalisababishwa na jinsi Shujaa ilivyo cheza katika michuano ya Hamilton, New Zealand ambako Kenya ilishinda mechi tatu naku shindwa katika mechi mbili.

Hata hivyo matarajio hayo yali zimwa kwa haraka kufuatia matokeo kadhaa mabaya ambayo Shujaa ilipata, nakusababisha kenya kumaliza michuano ya Sydney7s bila kushinda hata mechi moja.

Mashabiki wa shujaa, katika michuano ya Sydney 7s 2019
Mashabiki wa shujaa, waonesha hisia zao katika michuano ya Sydney7s 2019 baada ya Kenya kuondolewa katika michuano hiyo. Source: SBS Swahili

Mashabiki wengi ambao SBS Swahili ilizungumza nao, wali sikitishwa kwa jinsi Kenya ilivyo cheza katika michuano ya Sydney7s, hata hivyo wengi wao walikuwa na matarajio chanya kwa timu hiyo iliyo jawa vijana wengi chipukizi.

Jacob Ojee Nahodha wa Shujaa Kenya
Jacob Ojee Nahodha wa Shujaa Kenya, ndani ya uwanja wa michuano ya Sydney7s 2019 Source: SBS Swahili

Tulipo zungumza na nahodha wa Shujaa Bw Jacob Ojee, naye pia ali elezea masikitiko yake pamoja na machezaji wenzake katika michuano hiyo.

Bw Ojee aliwashukuru mashabiki kwaku endelea kuwa na imani na timu, pamoja naku washabikia na ali ahidi kuwa timu yake, ita fanyia kazi mafunzo waliyo pata katika michuano ya Sevens inayo salia.
Mashabiki wa shujaa, katika michuano ya Sydney7s 2019
Mashabiki wa shujaa, katika michuano ya Sydney7s 2019 Source: SBS Swahili
Matokeo mabaya ya Shujaa katika michuano ya Sydney7s hayaku vunja mioyo yawa Kenya kabisa, maana wali endelea kushabikia timu zilizo salia katika michuano hiyo.

New Zealand ili onesha umahiri wake uwanjani, ambako timu zake za wanaume na wanawake walinyakua ushindi wa michuano ya Sydney7s 2019.


Share

1 min read

Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS Swahili



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service