Ushindi huo ulipatikana kwa jasho baada ya mshambuliaji wao maarufu Sadio Mane, kushindwa kufunga penati katika dakika ya sita ya fainali hiyo dhidi ya bingwa mara saba wa Afrika Misri.
Hata hivyo Mane hakufa moyo na yeye na wachezaji wenza walionesha viwango vyao pamoja na vipaji, kwaku tawala fainali hiyo kwa muda mrefu hatakama hawakufanikiwa kufunga goli lolote katika muda wa masaa mawili ya mechi hiyo.
Upande wa pili wa fainali hiyo alikuwa Mo Salah, mchezaji ambaye kwa sasa anazingatiwa kuwa mchezaji bora wa soka duniani ambaye pia hucheza pamoja na Mane katika kikosi cha Liverpool, Uingereza. Hata hivyo, urafiki uliwekwa kando kila mmoja wao akitetea nchi yake katika mechi hiyo.
Hatma ya mechi hiyo iliamuliwa kupitia penati, ambapo wadau wengi waliwapa Misri matarajio yao kwa sababu walikuwa tayari wameshiriki katika mechi mbili kabla ambazo walishinda zote kupitia penati. Hata hivyo, bahati haikuwa upande wao, na baada ya mlinda lango Mendy kuokoa penati ya Misri, Sadio Mane alijikomboa nakufuta kosa lake la awali kwaku tuma kombora la penati katika wavu za mlinda lango wa Misri na sekunde chache baadae uwanja mzima uli lipuka kwa shangwe. Misri na Senegal zitakutana tena mwezi wa tatu, katika mechi mbili zaku amua timu gani itashiriki katika kombe la dunia baadae mwaka huu Qatar.
Share

