Tanzania yamlilia Rais Mstaafu Banjamin Mkapa

Afariki hospitalini baada ya kuugua, mamia kumuaga uwanjani

Late Banjamin Mkapa

Source: 2 eyez media

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli hapo jana kwa masikitiko makubwa alitangaza kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa kilichotokea usiku wa kuamkia jana taraehe 24 Julai 2020.

Mhe. Rais Magufuli alisema, Mhe Banjamin Mkapa alifariki dunia hosptalini jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akipatiwa matibabu.

Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania wote kuwa watulivu na wastahimilivu baada ya kupokea taarifa za kuondokoewa na mpendwa wao Mhe. Benjamini William Mkapa.

Mhe. Magufuli alisema, Watanzania walipkee hilo, wamepata msiba mkubwa na waendelee kumuombea Mzee wao Mstaafu Banjamin Mkapa ambaye ametangulia mbele za haki.

Kufuatia msiba huo mkubwa huo, Rais Magufuli alitangaza siku 7 za maombolezo ya Kitaifa kuanzia Ijumaa tarehe 24 Julai, 2020.

Mwili wa Marehemu Benjamin William Mkapa unatarajiwa kuzikwa Jumatano ijayo kijijini Mpaso wilayani Masasi mkoani Mtwara.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa, shughuli za kuaga zitafanyika kwa siku tatu kuanzia Jumapili na zitafanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

 

 


Share

Published

By Frank Mtao

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service