Tanzania yaomboleza kifo cha Rais John Pombe Joseph Magufuli

Katika hotuba yake fupi kupitia runinga ya taifa, Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ame tangazia taifa kwa masikitiko kifo cha Mhe Dkt Rais John Magufuli.

Mhe Dkt Rais wa Tanzania John Pombe Joseph Magufuli

Mhe Dkt Rais Magufuli awapungia mkono wananchi, katika tukio lakitaifa Dodoma, Tanzania Source: AAP

Katika hotuba yake fupi, Makamu wa Rais alisema kwamba:

"Tarehe 17 Machi 2021 majira ya saa kumi na mbili jioni, tume mpoteza kiongozi wetu shupavu, Rais wa Muungano wa Jamuhuri ya Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli."

Aki elezea kilicho sababisha kifo cha Rais, Mhe Hassan alisema:

"Alifariki kwa maradhi ya moyo katika hospitali ya Mzena, jijini Dar es Salaam akipatiwa matibabu. Mhe Rais Magufuli alilazwa tarehe 6 Machi 2021, katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete, kwa tatizo la moyo la mfumo wa umeme ambalo alikuwa nalo kwa zaidi ya miaka 10." Image

Mhe Hassan anaye tarajiwa kurithi wadhifa wa mwendazake, ameongezea kuwa mipango ya mazishi inafanywa na Tanzania itakuwa katika kipindi cha maombolezo kwa siku 14 na mbendera zitapepea nusu mlingoti.

Mhe Dkt Rais John Pombe Joseph Magufuli, ni miongoni mwa viongozi kadhaa katika serikali ya Tanzania walioga dunia katika siku na wiki chache zilizopita, baadhi wakiripotiwa kufa kwa ungonjwa wa Coronavirus. Mhe Dkt Rais Magufuli ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 61.

SBS Swahili itakupa taarifa zaidi kuhusu tukio hili, punde tutakapo zipokea.

   


Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service