Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Thiago kuukosa mtanange dhidi ya Dortmund

Thiago Alcantara leo usiku atakosa kushiriki kivumbi kati ya timu yake Bayern Munich ikichuana vikali na Borussia Dortmund

Thiago
(Bongarts) Source: Getty Images

Kocha wa Bayern Hansi Flick amekiri kuwa kiungo huyo hatokuwepo leo kwenye mchezo utakaopigwa Signal Iduna Park baada ya kulazimishwa kukosa mazoezi ya Jumatatu. 

"Thiago hakufanya mazoezi," Flick alisema. 

"Kwa bahati mbaya, ameondolewa kwenye mchezo huu. Siri ya mwisho juu ya kikosi kamili, ningependa kubaki nayo mwenyewe."

Thiago amekwisha cheza mara 23 katika ligi hiyo kwenye msimu huu lakini alikaa nje kwenye mchezo wa Jumamosi iliyopita kutokana na maumivu ya nyonga, ambapo Bayern iliichakaza Eintracht Frankfurt kwa mabao 5-2.


1 min read

Published

Presented by Frank Mtao

Source: SBS The World Game


Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now