Watoto wawili ni miongoni mwa watu 41 waliouawa katika ajali ya ndege ya Urusi iliyoteketea kwa moto

Watu arobaini na moja kati ya watu 78 wameuawa, ikiwa ni pamoja na watoto, walipanda ndege ya abiria aina ya Aeroflot ambayo iliwaka moto baada ya kutua uwanja wa ndege wa Moscow.

A Sukhoi Superjet 100 of Russian airline Aeroflot burning at Moscow's Sheremetyevo airport, Russia, 05 May 2019.

A Sukhoi Superjet 100 of Russian airline Aeroflot burning at Moscow's Sheremetyevo airport, Russia, 05 May 2019. Source: AAP

Ndege ya abiria ililipuka moto siku ya Jumapili hivyo ikafanya kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Moscow wenye pilika nyingi, na kuua watu angalau 41 kulingana na taarifa za maofiosa.

"Ndani ya ndege kulikuwa na watu 78 ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa ndege hiyo," Kamati ya Upelelezi ilisema katika taarifa, mapema ilitangaza kuwa angalau wawili wa waliofariki walikuwa watoto.

"Kwa mujibu wa taarifa za sasa ambazo wachunguzi wanazo, watu 37 walinusurika"

Video ya kushangaza iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ilionyesha ndege hiyo ya Kirusi ya Aeroflot, ikiwaka moto na moshi mweusi ukifuka kutoka kwenye sehemu kuu ya ndege hiyo, ilitua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sheremetyevo.

Abiria walionekana kuruka kupitia milango ya dharura na miteremko ya maboya mbele ya ndege kukimbia kutoka ndege iliyokuwa ikiwaka moto huku moshi mkubwa mweusi ukifuka kuelekea angani.


Share

Published

By Frank Mtao
Presented by Frank Mtao
Source: AFP, SBS

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service