Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Umtiti aiangusha Ubelgiji na kuipeleka Ufaransa fainali ya Kombe la Dunia

Samuel Umtiti alikuwa shujaa asiyetarajiwa wakati Ufaransa ikiingia fainali za Kombe la Dunia la FIFA 2018 kwa mara ya tatu katika kipindi cha miaka 20 kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ubelgiji mjini St Petersburg leo Jumatano kwa saa za Australia (AEST).

Umtiti

(Getty Images) Source: Getty

Beki huyo, alipiga kichwa mpira wa kona iliyopigwa na Antoine Griezmann katika dakika ya 51 hivyo kufanya kuwepo mtanange wa mataifa ya Ulaya ambapo kikosi hicho maarufu kama Les Bleus kitaelekea mjini Moscow kwa mpambano kati ya Kroatia au Uingereza.

Walinda mlango Hugo Lloris na Thibaut Courtois wote walifanikiwa kuokoa michomo mingi katika kuhakikisha mchezo huo mkali ubaki bila kufungana.

Hata hivyo, Umtiti akaibuka mapema kwenye kipindi cha pili, kwa kufunga goli lake la tatu la michezo ya Kimataifa.

Umtiti header sends streetwise France into World Cup final
(Reuters) Source: Reuters

Ubelgiji walijitahidi kwa nguvu zote kusawazisha lakini akajikuta Roberto Martinez akiangalia kikosi chake kikiadhibiwa kipigo chao cha kwanza tangu michezo 25 hivi, hivyo kuondoa matumaini yao ya kushinda kombe hilo kwa mara ya kwanza katika historia yao kwa vijana wanaofahamika kama kizazi cha dhahabu kushindwa kufurukuta.

Kikosi ambacho kilipoteza ubingwa wa Ulaya mwaka 2016 kwenye ardhi ya nyumbani Ufaransa, watakuwa na lengo la kufanya vizuri mwaka huu nchini Urusi na hivyo kurudisha heshima iliyowekwa na kikosi cha mwaka 1998 ambacho kilimjumuisha Didier Deschamps, ambaye huenda akafuata nyayo za Mario Zagallo na Franz Beckenbauer kwa kushinda kombe la dunia kama mchezaji na pia kocha.


1 min read

Published

By sbs

Presented by Frank Mtao

Source: SBS The World Game



Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now