Vitongoji 4 jijini Sydney, vyawekewa vizuizi vikali vya COVID-19

Kuanzia usiku wa manane wa Ijumaa, wakaaji katika vitongoji vinne jijini Sydney, watawekewa amri yakubaki nyumbani.

Sydney areas put into lockdown after NSW records 22 new COVID-19 cases

Jimbo la New South Wales larekodi kesi mpya 22 za coronavirus Source: ABC Australia

Vizuizi vimewekwa kwa mikusanyiko na amri yakuvaa barakoa katika maeneo pana ya Sydney imerejeshwa tena. Mamlaka wa afya wanaendelea kuongeza juhudi zaku dhibiti aina ambukizi sana ya coronavirus kwa jina la Delta, makatazo hayo yakutoka nje pamoja na amri yakuvaa barakoa, inatarajiwa itasalia hadi 2 Julai 2021 kwa maeneo pana ya Sydney pamoja na maeneo kama; Central Coast, Blue Mountains, Wollongong na Shellharbour.

Mtu yeyote anaye ishi au anaye fanya kazi katika vitongoji vya Woollahra, Waverley, Randwick, na City of Sydney, ataruhusiwa tu kutoka nyumbani kwake akiwa na sababu muhimu. Baadhi ya sababu hizo ni: kununua vifaa muhimu, kufanya kazi au kwenda shuleni kama kazi hiyo au hawezi somea nyumbani, kupokea au kutoa huduma, na kufanya mazoezi katika vikundi vya watu 10 au wachache.

Vizuizi hivyo vitasalia hadi usiku wamanane wa 2 Julai 2021.


Share

Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migearano

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Vitongoji 4 jijini Sydney, vyawekewa vizuizi vikali vya COVID-19 | SBS Swahili